vita iraq vyawatesa watoto | maendeleo media
BREAKING NEWS
Loading...

Wednesday 21 June 2017

vita iraq vyawatesa watoto



Shirika la Kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limeonya kwamba watoto takriban milioni tano nchini Iraq wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.

Shirika hilo limesema watoto wa nchi hiyo hususan wale wote walio katika mji wa Mosul, ambako majeshi ya Iraq yanapambana vikali na wapiganaji wa Islamic state, wamejikuta katika ghasia na umasikini usio na mwisho.

Takwimu zilizooneshwa na UNICEF zinaonesha kuwa nusu ya wagonjwa wanaotibiwa katika vituo vya watu wenye maradhi ya wasiwasi na kuchanganyikiwa kutokana na hofu, (magonjwa mabaya ya akili) magharibi mwa Mosul ni watoto.

Kwa mujibu wa ripoti, watoto wapatao laki nane nchini Iraq kote, wamepoteza mzazi japo mmoja.

Mashirika ya misaada yanasema fedha zaidi zinahitajika haraka kuweza kusaidia kuwalinda watoto wa Iraq, kutokana na mapigano hayo.

google+

linkedin